Categories
Dondoo za afya

Kwanini unaumwa kichwa bila kupona

Nini husababisha Maumivu ya kichwa?

Makala hii itakupa maelekezo jinsi gani uweze kugundua chanzo cha maumivu ya kichwa yanayokupata, hii itakusaidia kuamua njia sahihi ya kutibu tatizo lako pasipo kukimbilia kumeza vidonge vya kupunguza maumivu ambavyo vina madhara makubwa kama vikitumika kwa muda mrefu pasipo ushauri wa daktari.

Yafuatavyo ni Baadhi ya mazingira yanayopelekea upate Maumivu ya Kichwa

  1. Mwili Kupungukiwa na maji

    Watu hupata maumivu ya kichwa pale mwili unapopungukiwa na maji, kama unapata maumivu ya kichwa baada ya kutapika sana, kutokwa na jasho jingi au mafua ya muda mrefu ni wazi kwamba unahitaji kunywa maji mengi ili kuondoa tatizo lako.
    Kama ni mtu wa mazoezi sana na huna tabia ya kunywa maji ya kutosha mwili utapungukiwa na maji na ni lazima kichwa kitauma. Kwenye majira ya joto sana hupelekea mwili kutoa jasho jingi na kuishiwa maji. Kumbuka kwamba mwili unahitaji maji ya kutosha ili kuendesha shuguli za ndani.

  2. Mwanga wa simu, coumputer na vifaa mbalimbali

    Kuangalia TV kwa muda mrefu ama matumizi makubwa aya simu yanafanya misuli ya macho kukaza na hatimaye kupelekea macho kuuma., vitu vingine vinavyopelekea kukaza kwa misuli ya macho ni kama  kutazama kitu kimoja ama upande mmoja kwa muda mrefu mfano unapoendesha gari na kusoma, Kukaa kwenye mazingira yenye mwanga mkali sana ama mwanga hafifu, mwili kuwa mchovu na ukavu wa macho.
    Kutatua changamoto hii ya kukaza kwa misuli ya macho hakikisha badili uelekeo wa mahali unapoangalia kila mbaada ya dakika 20. kama kuna kazi inakutaka utumie muda mwingi kuifatilia kwa macho basi hakikisha unabalansi na shughuli zingine ambazo zinahitaji pia matumizi ya macho.
    Hakikisha kifaa chako kama simu, computer ama televisheni kipo mbali kuanzia cm 30 , simu unapotumia iweke katika usawa wa chini kidogo na level ya macho. Kama tatizo ni kubwa ongea na dactari wako wa macho akushauri aina ya miwani ya kutumia ili kujikinga na miale ya mwanga.

  3. Vichocheo vya mwili (hormones)

    Kupungua kwa uzalishaji wa homoni ya estrogen huchangia mabadiliko ya utoaji wa chemikali kwenye ubongo zinazochangia maumivu ya kichwa. Inatokea zaidi kwa wanawake wanapokuwa kwenye kipindi cha hedhi.
    Wanawake waliokoma hedhi ama wanaokaribia kukoma hedhi hupata pia maumivu ya kichwa kwa estrogen hupungua kwa kiasi kikubwa.
    Matumizi ya njia ya kuzuia mimba na tiba ya homoni za kutegenezwa maabara (hormone replacement therapy) huchangia kuongezeka ama kupungua kwa baadhi ya homoni na kisha kupata maumivu ya kichwa.
    Kwa wajawazito homoni ya estrogen huongezeka na kupelekea maumivu ya kichwa, baadhi ya wanawake maumivu haya huisha ndani ya kipindi kifupi, wengi hupata maumivu haya kwenye miezi ya kwanza ya mimba. baada ya kujifungua kiwango cha estrogen hushuka tena.

  4. Ukaaji wa mwili

    Ukaaji na ulalaji mbovu unapelekea presha kubwa eneo la juu nyuma ya mwili na kwenye mabega na hivo kupelekea maumivu ya kichwa. Maumivu unayoyapata baada ya kulala ama kukaa au kusimama kwa muda flani ni matokeo ya mwili kutobalansi.

  5. Kutoshugulisha mwili

    Mazoezi ya mwili ikiwemo kukimbia, kuendesha baiskeli, au squats husaidia mwili kutoa kemikali ambazo ni pain killer mfano endorfins. Watu wasiofanya mazoezi na wanaotumia muda mwingi wamekaa pasipo kushughulisha miili ni wahanga wa kuumwa kichwa. Hakikisha unaweza ratiba walau mara 3 kwa week kufanya mzoezi.

  6. Matumizi ya dawa

    Matumizi ya baadhi ya dawa ya kupunguza maumivu kwa muda mrefu badala yake huleta maumivu ya kichwa .Matumizi ya dawa ambazo zipo kwenye kundi la nonsteroidal anti-inflammatory drugs (NSAIDs) husababisha tatizo kuwa baya zaidi.

  7. Msongo wa mawazo.

    Msongo wa mawazo hupelekea misuli yako kukaza na hivo kubadili namna ubongo unavotoa kemikali hadi kupelekea maumivu ya kichwa. kama wewe ni muhanga wa stress unaweza kusoma vzuri kuhusu namna sahihi za kudeal na msongo wa mawazo hapa.

  8. Kelele

    Kukaa kwenye mazingira yenye kelele nyingi kwa muda mrefu hisababisha kuumwa kichwa .

Njia gani utumie ili kupunguza maumivu ya kichwa kabla ya kumwona Dactari.

  • Tumia kipande cha barafu kwenye mfuko weka kwenye eneo la mbele la kichwa.
  • Kunywa maji ya kutosha walau glass 8 kwa siku
  • Fanya mazoezi madogo ya kutembea hasa kutembea peku kwenye mchanga wa bahari
  • Kaa mbali na eneo lenye kelele na mwanga mkubwa, tafuta eneo lililotulia

Ni muda gani unatakiwa kumwona dactari.

Endapo utapata dalili zifuatazo hakikisha unamwona dactari haraka

  • Maumivu ya muda mrefu pasipo kupata nafuu
  • Maumivu ya kichwa yanayoambatana na homa
  • Kupungua kwa uwezo wa kuona shingo kuwa ngumu
  • Kushindwa kutembea na tatizo kwenye kuongea
  • Kukosa nguvu ama kutetemeka kwa eneo moja la mwili
    Kumbuka ni muhimu kumwona dactari endapo dalili za kuumwa kichwa zitendelea zaidi pamoja na kwamba umetumia njia za kupunguza maumivu haya.

Tumia Mafuta ya lavender kutuliza kichwa

Mafuta ya lavender au mrujuani ni moja ya mafuta yanayotumika zaidi kwenye kundi la (essential oil) lakini faida zake ziligunduliwa kwa zaidi ya miaka 2500 iliyopita katika kutibu magonjwa kichwa na msongo wa mawazo.

Matumizi:Kutuliza kichwa kuuma pakaa matone kidogo eneo la masikio na pua, na pia dondosha matone mawili kwenye mto wa kulalia. Usimeze tena dawa za maumivu kwani zitakuletea magonjwa ya figo na ini bure. badala yake tumia haya mafuta ya asili.

Mafuta ya levender yamekuwa adimu sana kutokana na uwezo wake mkubwa wa kutibu. Fika ofsini hapa Magomeni Mwembechai upate mafuta haya ambayo ni original na asili.

Gharama ya mafuta ni sh 40,000/= Tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254 kupata tiba

Share and Enjoy !

Shares
Categories
Dondoo za afya

Kwanini Unanuka mdomo

Leo nataka kushea na wewe njia zangu rahisi jinsi gani uweze kutibu tatizo la kunuka mdomo, ikiwemo lishe na virutubisho vya kutumia katika program yako.

Kunuka mdomo ni hali ambayo kila mtu haipendi na moja ya matatizo ambayo watu huona aibu sana kuelezea. Lakini nataka nikwambie rafiki yangu unaesoma makala hii kwamba ukitaka kutibu tatizo la kunuka mdomo  inahitajika kufahamu chanzo cha tatizo hili.

Kikawaida kunuka mdomo kunasababishwa na kumea kwa bakteria wabaya kwenye mwili wako. Lkini kunuka mdomo ambako ni sugu na imekuwa ni hali ya muda mrefu husababishwa ukuaji kupita kiasi wa fangasi aina ya Candida kwenye mwili. Baadhi ya vyakula kama kitunguu saumu vinaweza kukupa ahueni ya muda mfupi . Nependa ufahamu kwamba kunuka mdomo si tu kwamba inaleta karaha bali pia ni kiashiria kwamba una tatizo kubwa la kiafya

Sababu Za Kunuka Mdomo

Karibu kila mmoja wetu hupata tatizo la kunuka mdomo katika muda fulani kwenye maisha yake. Wakati mwingine kisababisho kinaweza kuwa ni chakula ulichokula au aina ya bacteria wanaopatikana kwenye mdomo wako.

Harufu mabaya kwenye mdomo hutokea nyuma ya ulimi, kwenye koo na kwenye tonsils. Huku ndiko bacteria wabaya wanakozailiana na kutoa kemikali za Sulphur ambazo ndizo huleta harufu mbaya. Kwahiyo harufu mbaya mdomoni inaweza kusababishwa na ulaji wa vyakula vyenye Sulphur kwa wingi.

Ambapo kikawaida harufu hii huisha baada ya chakula kuchakatwa. Harufu mbaya mdomoni ya muda mrefu ni kiashiria cha uwepo wa tatizo la kiafya ambapo yaweza kuwa ni

  • Kutofanya usafi wa mdomo kwa makini
  • Lishe duni isiyo na virutubisho vya kutosha
  • Magonjwa ya fizi
  • Kuoza kwa meno na
  • Mataizo mengine ya kiafya kama kisukari au magonjwa ya ini

Ulaji wa vyakula hivi inaweza kuwa sababu ya kunuka mdomo kutokana na kwamba vizalisha kemikali nyingi ya Sulphur, vyakula hivi ni kama

  • Kitunguu maji na  kitunguu saumu: vyakula hivi huleta harufu kali zaidi hizo unatakiwa kuvitumia kwa tahadhari.
  • Vyakula vya sukari: sukari hupelekea kuoza kwa meno na kupelekea harufu mbaya mdomoni
  • Vinywaji vilivyosindikwa kama soda.

Hatua Tano za Kutibu tatizo la Harufu Mbaya Mdomoni

  1. Epuka kutumia vyakula vya sukari kwa wingi na nafaka kupita kiasi: hii ni ahtua ya kwanza katika kuelekea kuondoa harufu mbaya mdomoni, ambapo tunalenga katika kufata lishe ambayo ina kiwango kidogo cha sukari na nafaka. Vyakula hivi ni kama mikate, wali na bidhaa zingine za ngano. Hivo unapokula zaidi wanga fahamu kwamba unaenda kuvunjwa vunjwa na kubadilishwa kuwa katika mfumo wa sukari kitu ambacho ni mbolea kwa ukuaji wa fangasi na bacteria wabaya kwenye mwili wako
  2. Tumia vyakula vya mafuta zaidi(healthy fats) : badala ya kula wanga na sukari basi hakikisha unakula zaidi vyakula mafuta mazuri, mfano wa vyakula hivi ni kama parachichi, nazi, nyama , mayai na karanga. Mafuta ya nazi ya nazi yana lauric na Capric acid ambazo ni ni antibacterial yaani zinaua bacteria wabaya.kama una matatizo ini, mfuko wa bandama na figo.
  3. Tumia virutubisho zaidi. Unaweza kutembelea katika stoo yetu kwa kubonyeza hapa
  4. Tumia zaidi limau: limau na maji husaidia kwa kiasi kikubwa katika kuondoa harufu mbaya mdomoni. Unaweza kukata limau kisha ukanyonya maji yake, au ukaminya maji ya limau kwenye glass yenye maji kisha kunywa maji haya na yabaki mdomoni kwa muda wa dakika 10 kisha tema.

Kunywa maji ya kutosha: mdomo unapokuwa mkavu basi huongeza hatari ya kutoa harufu mbaya, kutokana na kwamba ukavu wa mdomo unapelekea kuzaliana kwa bacteria wabaya.

Coconut Oil Pulling

coconut oil pulling

Coconut oil pulling ni mja ya njia murua kabisa ya kusafisha bacteria wabaya mdomoni mwako na kukuacha na harufu nzuri ya kinywa sikuzote. ni njia salama na ya asili isiyohitaji matumizi ya kemikali mbaya wala dawa ambazo zina madhara makubwa.

Nimekuwa nikishauri mamia ya watu na wamefanikiwa kuondoa adha hii ya kunuka mdomo kupitia Coconut oili pulling, wewe pia unaweza kuwa mmoja wa mashuhuda wetu kama tu utazingatia kwa makini step za kufuata.

Uchafu na Vimelea Hutolewa Nje kupitia mafuta

Coconut oil pulling kama jina lake lilivyo ni kitendo cha kuvuta uchafu na bacteria ka vile sabauni inavyonyonya uchafu kwenye nguo wakati wa kufua nguo. Lakini kwenye upande wa kinywa unanyonya bacteria na uchafu kwenye meno kwa kutumia mafuta ya kupikia ya nazi.
Wenzetu wachina na nchi zingine kama India wamekuwa wakitumia njia hii tangu enzi za zamani katika kutibu matatizo kama

Kuoza kwa meno, kuondoa harufu mbaya kwenye kinywa, kuponya fizi zinazotoa damu, kuzuia magonjwa ya moyo, Kupunguza mcharuko mwilini (inflammation), Kusafisha meno kuwa meupe, Kuzuia magonjwa ya fizi, Kutibu lips kavu, Kuimarisha fizi na Kuondoa chunusi

Hatua 5 za Kufanya Coconut Oil Pulling

  1.  Hakikisha unafanya oil pulling asubuhi unapoamka kabla ya kula na kunywa kitu chochote
  2. Chukua kijiko kimoja au viwili vya mafuta ya kupikia ya nazi kisha weka mdomoni, anza kuzungusha ulimi na kuyasambaza mdomo wote taratibu kwa dakika 10 mpaka 20
  3. Baada ya muda huu tema uchafu wote bila kumeza hata kidogo kisha safisha mdomo na maji, unaweza kutumia maji yenye chumvi ili kuondoa mafuta yote. na hakikish usiteme kwenye sink tema nje ili kuzuia kuziba kwa mafuta kwenye sinki
  4. Brush meno yako kama kawaida
  5. Rudia kitendo hiki mara 3 mpaka 5 kwa week kupata matokeo mazuri zaidi.

Tiba Kupitia mafuta ya Peppermint

Mafuta ya mnanaa ama peppermint yanapatikana kupitia majani ya mmea wa mnanaa (Mentha piperita). Mmea huu hutumika hasa majumbani kama tiba asili ya matatizo ya tumbo.

Mafuta ya peppermint ni tiba asili na salama kwa changamoto ya kunuka mdomo na mezo kuoza. Huhitaji tena kuagiza nje ya nchi, tumekuletea mafuta salama yasiyochakachuliwa. Anza leo kutumia urudishe furaha yako.

Gharama ya Mafuta ya Peppermint ni Tsh 40,000/= Tuandikie kwa whatsapp no 0678626254

Share and Enjoy !

Shares
Shares