Categories
Urembo wa ngozi

Njia Asili za Kuondoa Michirizi kwenye ngozi

kuondoa michirizi kwenye ngozi
michirizi kwenye ngozi

Wanawake wengi kwa sasa wanatafuta njia gani salama za kuondoa michirizi kwenye ngozi. Michirizi na mikunjokunjo kwenye ngozi ya mapaja, tumbo na kwenye mikono ni tatizo linalowatesa zaidi wanawake. Kwani wengi wanahangaika ili kuondokana na tatizo hili bila mafanikio. Pamoja na kutumia vipodozi na cream mbalimbali bado tatizo halijaisha.

Tatizo linapelekea wadada kuona aibu, kushindwa kujiachia na kutovaa nguo wanazozitaka kwa kuogopa mikunjokunjo kuonekana.  Makala yangu ya leo itaangalia tatizo kwa upana wake na kukupa mpangilio wa lishe na ushauri wa kina. Pamoja na njia za asili za kutibu tatizo lako ili ufurahie urembo wako wa mwili, karibu.

Michirizi au cellulite ni kitu gani?

Cellulite ni mwonekano wa mikunjokunjo na mistari kwenye ngozi ya mwili. Mistari hii hutokea zaidi kwenye eneo la tumbo, chini ya mikono, kwenye mapaja na matako. Michirizi hutokea zaidi kadiri umri unavoenda. Baadhi ya vitu vinavyoletekeza mikunjokunjo kwenye ngozi ni pamoja na kuvurugika kwa homoni, pamoja na kutokufanya mazoezi.

Wanawake wanapata zaidi Michirizi kuliko Wanaume

Tatizo hili huwatokea zaidi wanawake kuliko wanaume ambapo kutokana na unene. Unene kupita kiasi hupelekea leya ya ndani yenye mafuta (fat globules) kuwa na msuguano na tishu za ngozi na hivo kupelekea mikunjokunjo na michirizi kwenye ngozi.

Tafiti zinasema kwamba asilimia 80 ya wanawake wana tatizo hili la cellulite. Ambapo wengi wanalipata kadiri wanavozeeka kwa ngozi kupungua uwezo wa kuvutika na kusababisha nyama kuanguka na kuleta mikunjokunjo.

Kuwa na michirizi siyo tatizo kubwa kiafya ndio maana wengi huliacha kama lilivyo bila kushughulika nalo. Lakini kama wewe ni mwanamke unayependa urembo na unapenda kujiachia maeneo kama beach na sehemu za wazi basi hiki kitakuwa kikwazo sana. Maana utaogopa kuonekana na watu kwamba ngozi yako ina kasoro ndio maana nimeandika makala hii ikusaidie.

Nini kinasababisha Michirizi Kwenye Ngozi

Mazingira hatarishi na sababu zinazochangia upate mikunjokunjo na michirizi kwenye ngozi ni pamoja na

  • lishe mbovu
  • mwili kubakiza maji tumboni (fluid retention ambapo wakati mwingie hupelekea tumbo kujaa gesi)
  • damu kutozunguka vizuri
  • udhaifu wa tishu zenye collagen na kuepelekea kujikunja kiurahisi
  • mabadiliko ya homoni
  • mwili kukosa mazoezi na kutoshugulika
  • msongo wa mawazo kupita kiasi ambao hupunguza uzalishaji wa collagen: collagen ni kiungo kilichosheni protini ambacho kinatengeneza shape na tishu za ngozi, hivo kufanya ngozi ya mtu kuonekana bado changa.
  • historia ya magonjwa mfano magonjwa ya autoimmune, kisukari, watu wanaovuta sigara na wenye alegi/mzio.

Sasa umejifunza jinsi sababu za kimaisha zinavoharibu mwonekano wa ngozi yako na tayari umejua chanzo cha tatizo lako kuwa ni kwenye lishe. Ni wazi sasa kwamba dawa na cream za kupata kwenye ngozi au mikanda ya kuvaa ili upunguze michirizi siyo suluhisho salama na la kudumu. Bali unatakiwa kubadili mtindo wa maisha  kwenye lishe na kuweka ratiba ya mazoezi.

Tiba Asili ili Kuondoa Michirizi na Mikunjokunjo kwenye Ngozi Yako

Hizi ni njia zangu 5 zitakazokusaidia kuondoa shida ya michirizi.
Angalizo: Kama wewe unataka njia za haraka haraka basi hutazipata hapa. Maana ninaelekeza namna ya kubadili mtindo wa maisha ili uepuke tatizo miaka yote, na itachukua muda kupata matokeo.

1.Kula Lishe Bora

Kama tulivosoma pale juu kuna uhusiano mkubwa kati ya uzito mkubwa na kitambi na kupata mikunjokunjo. Hivo punguza vyakula vya wanga na sukari na kula zaidi vyakula vya mafuta kama nyama, parachichi, nazi na mafuta ya nazi, samaki nk. Weka ratiba ya kupunguza unene wako uliopitiliza kwa kufanya mazoezi na kushugulisha mwili wako.

2.Tumia Collagen ya Kutosha

Kama tulivojifunza mwanzoni ni kwamba tishu za ngozi zimetengenezwa kwa protini za collagen. Kwahiyo kama ngozi yako ipo imara basi utapunguza uwezekano wakupata mikunjokunjo. Collagen ni protini inayopatikana kwa wingi kwenye ngozi na husaidia kuvutika na kufanya ngozi kuwa hai na laini.

Chanzo kizuri cha Collagen ni kunywa supu ya mifupa (bone broth) . Supu ya mifupa ina amino acid kwa wingi ambazo hutengeneza collagen. Collagen iliyopo kwenye Supu ya mifupa  husaidia kuimarisha tishu za ngozi na kuondoa tatizo la cellulite.

3.Tumia virutubisho

Virutubisho vya kuondoa mikunjokunjo kwenye ngozi na michirizi (anti-cellulite suppliments): Unaweza kufika ofsini kwetu ukatumia virutubisho kama royal gel na sipiriluna vikakusaidia kupambana na tatizo lako bila kikwazo.

4.Fanya mazoezi kila mara

Mazoezi ni njia nzuri sana pale unapotaka kupunguza uzito. Tumeona pale juu athari za uzito mkubwa na kitambi kwenye kupata mikunjokunjo, pamoja na kula lishe nzuri ni muhimu sasa uweke ratiba ya kufanya mazoezi walau mara tatu kwa week.

5.Tumia mafuta asili ya nazi kwenye kutibu ngozi yako.

Unaweza kutumia mafuta halisi ya nazi kwa kupaka kwenye ngozi yako baada ya kuoga. Kumbuka cream za madukani zinaweza kuwa ghali na hatari kwa afya yako kwa maana zina kemikali na metali nzito ambazo ni sumu kwa afya ya ngozi.

Maelezo ya Mwisho pale Unapopambana na michirizi+mikunjokunjo

  • Cellulite ni mwonekano wa mikunjokunjo kwenye ngozi na hii ni kutokana na kusuguana kwa tabaka la mafuta na tishu za ngozi
  • Sababu zinazopelekea upate mikunjokunjo kwenye ngozi ni pamoja na uzito mkubwa, lishe mbaya, kubakiza maji ama mwili kukosa kabisa maji, matatizo kwenye usafirishaji mwilini na udhaifu wa tishu zenye collagen kwenye ngozi
  • Kupunguza uzito, kula vyakula asili vyenye kambakamba na kufanya mazoezi ,  husaidia kupunguza sana tatizo la cellulite.

Mafuta ya lavender yanasaidia kuondoa michirizi

lavender oil

Mafuta ya lavender au mrujuani ni moja ya mafuta yanayotumika zaidi kwenye kundi la (essential oil) lakini faida zake ziligunduliwa kwa zaidi ya miaka 2500 iliyopita katika kutibu magonjwa na matatizo ya ngozi.

Matumizi ya mafuta ya lavenda kwa kupakaa kwenye ngozi huzuia na kuondoa chunusi na matatizo mengine ya ngozi kama madoa, michirizi, mikunjokunjo na pia kupunguza kasi ya kuzeeka kwa ngozi.

Mafuta ya levender yamekuwa adimu sana kutokana na uwezo wake mkubwa kupambana na matatizo ya ngozi. Fika ofsini hapa Magomeni Mwembechai upate mafuta haya ambayo ni original na asili. Gharama ya mafuta ni sh 40,000/=

Tuandikie whatsapp kwa namba 0678626254 kupata tiba ya tatizo lako

Soma makala inayofuata kuhusu: Kubana tumbo baada ya kujifungua

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *