Hatua tano za kurudisha nguvu za kiume

nguvu za kiume
mahusiano

Napenda kukukaribisha tena katika jukwaa langu la afya yako. Leo tutajifunza tatizo ambalo limekuwa ni kubwa sana kupita kiasi kwa kila mwanaume kwa sasa. Tatizo linaloyumbishana ndoa na mahusiano pia. Changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume , ambayo inajumuisha kushindwa kurudia tendo, kuwahi kumaliza na uume kusimama legelege.

Usiwe miongoni mwa watu wenye upungufu wa nguvu za kiume. Yote hayo utayaepuka kwa kufuata ushauri huu ulio badili maisha ya watu wengi na bado elimu hii inaendelea kutoa shuhuda kwa kila mtu aliyekuwa na tatizo hili.

Historia ya Tatizo la Upungufu wa Nguvu za kiume

Tatizo la nguvu za kiume hapo zamani za kale na tafiti za kisayansi zinaonesha ni matokeo yanayotokea uzeeni. Yaani  kupungua uwezo wa tendo ni jambo la kawaida kwa umri mkubwa. Kwa kawaida binadamu hastahili kuzeeka na magonjwa.

Tunazeeka na magonjwa kwa sababu tunayasababisha sisi kutokana na aina ya maisha tunayoishi. Tunasahau kuwa afya sio hazina ya milele, unatakiwa kuiheshimu, kuilinda na kuimarisha ili uje ufurahie uzee wako usio na magonjwa.

Upungufu wa nguvu za kiume kwa vijana

Najua kuwa hadi sasa ukifanya tafiti vijana wa umri wa miaka 20 hadi 30 ndio wanao ongoza kwa kusumbuka na matatizo haya ya nguvu za kiume. Tofauti na matarajio yetu wote kuwa tatizo hili tunasoma kuwa linawapata wazee. Swali la kujiuliza kwa nini sasa vijana tena katika umri mdogo?

Ndio maana nimeamua kukuandikia makala hii. Ambapo kama ni miongoni mwa watu wanaosumbuka hili tatizo nina uhakika tatizo lako utapata suluhisho kutokana na elimu hii. Pia najua unaweza ukawa na mchumba wako, unavumulia mengi kuhusu tatizo hili la mwenzi wako.

Upungufu wa nguvu za kiume huleta hofu na mawazo

Usiwe mkimya kwani inahitaji utashi wa juu sana kumweleza mwenzi wako kuhusu hili swala. Kwani upungufu wa nguvu za kiume unasababisha msongo wa mawazo . Mbali na hivyo husababisha kutokujiamini na woga wa kuwa na mwanamke.

Wengi wamejaa wasiwasi na hofu kubwa ya kugunduliwa na mwezi wake kuwa ana tatizo hilo. Na wengi wao ni woga sana kutogunduliwa tatizo hilo. Ndio maana inapofikia hatua mwenza wako umembaini ni mara chache sana atakubali kuwa kweli hujamfiskisha kileleni kwa kuogopa kwamba atakukwaza. Kwa nini usumbuke na matatizo kama haya wakati tiba ipo?

Usiendelee kusumbuka na tatizo hili kwani umeumbiwa maisha ya furaha na Mungu. Ni haki yako kufurahia tendo la ndoa kila siku. Anza leo kushughurikia tatizo kabla halijawa sugu kwa kusoma zaidi makala hii.

Nini husababisha upungufu wa nguvu za kiume.

Katika mwili wa binadamu kuna vichocheo aina ya testosterone ambavyo hutolewa. Malengo ni kuimarisha utendaji kazi wa ubongo, ufanye kazi katika hali tulivu, kuondoa msongo na kuondoa mstuko wa aina yoyote.

Kazi zingine za homoni ya testosterone ni kuimarisha uwezo wa kufikiri, kuimarisha nguvu za kiume na hatimaye kufurahia tendo la ndoa. Kazi kubwa ya kichocheo hiki ni kuhakikisha mwili wako unakuwa katika hali tulivu kabisa kwa kuutuliza ubongo wako ndipo utafurahia ndoa yako.

Homoni zinategemeana

Sasa endapo kichocheo hiki kikivurugika kinasababisha vichocheo vingine kama insulin, leptin, cortisol, vichocheo vya ukuaji pia kuvurugika. Kwani matokeo ya hitililafu hii mwilini inasababisha  kupungukiwa nguvu za kiume. Kwa sababu vichocheo hivi vinafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa. Endapo kimoja tu kikivurugika vyote vinapoteza mwelekeo na tatizo kuwa sugu zaidi.

Napenda leo nieleze kwa kina kidogo namna gani nguvu za kiume zinapotea kutokana na mvurugiko wa vichocheo hivyo vikuu vitatu kama nilivyo vitaja hapo juu.

Homoni ya Testosterone

Kichocheo hiki ndio silaha ya mwanaume kwani ndicho kichocheo kinachokufanya uwe na sifa zote za kiume. Na ndicho kichocheo ambacho kinakufanya uwe imara katika tendo la ndoa. Upungufu wa kichocheo hiki kinasababisha kupungua kwa matamanio kwa jinsia tofauti, kupungua kwa nguvu za misuli yako kiutendaji, mafuta kurundikana ovyo mwilini.

Lakini pia ijulikane kuwa kichocheo hiki cha testosterone sio kwamba kinapatikana kwa wanaume tu, la hasha! Kichocheo hiki hata wanawake wanacho ingawaje kwa kiwango cha chini sana. Endapo kinapokuwa kimepungua kinaweza kumsababishia mwanamke kukosa matamanio kwa jinsia ya kiume wakati wa tendo la ndoa, kukosa nguvu ya misuli ya kuhimili tendo la ndoa ama kuchoka sana, kuongezeka uzito kupita kiasi na nyama uzembe pia kupunguza uwezo wako katika kufikiri na kumbukumbu.

Vitu gani hupunguza kiwango cha homoni ya testosterone.

Moja ya kisababishi kikubwa cha testosterone kushuka kiwango chake ni kwa sababu ya kuwepo na kizuizi cha insulin (insulin resistance). Hii inafanya kiwango cha insulin kuwa juu sana na kusababisha testosterone kushuka kiwango chake.

Moja ya sababu zinazopelekea kiwango cha insulin kuwa juu sana ni unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi kama soda na pia ulaji wa vyakula vyenye vionjo mbalimbali vitamu vilivyotengenezwa viwandani. Hivyo basi sukari inapokuwa katika kiwango cha juu sana kwenye damu inasababisha utolewaji wa insulin kwa kiwango cha juu pia kwenda kusawazisha sukari irudi kawaida.

Vyakula vya wanga na sukari kupita kiasi ni adui

Hivyo basi matumizi ya vyakula na vinywaji vya sukari nyingi vinafanya mwili upate kizuizi katika utendaji kazi wa insulin na hatimaye testosterone pia kushuka kiwango chake.

Najua umejifunza sasa kwa nini watu wanaotumia vyakula vya viwandani, vinywaji vya sukari nyingi,ulaji wa vyakula vyenye mafuta mabaya jinsi gani inasababisha vichocheo vyako kushuka kiwango na unaendelea kusumbuka sana. Napenda kukuambia kuwa siku zote watu hawaogopi vyakula vyenye sukari wanaogopa vyakula vyenye mafuta mengi.

Hii ni fikra potofu sana! Sugar is more addictive than heroin and cocaine. Kwa maana nyingine watu ni walevi wa vyakula na vinywaji vya sukari kupita hata ulevi wa unga,jambo linalohatarisha afya zao . Usihofu kama una tatizo hilo ujue tayari umeshaathiriwa na ulaji wa vyakula na vinywaji hivyo.

2.Homoni ya Insulin

Hiki ni kichocheo ambacho hutolewa na kongosho lako ili kwenda kusawazisha kiwango cha sukari mwilini mwako. Kazi kubwa ya maji haya ya insulin ni kuhifadhi nishati ya mwili kwa matumizi ya baadae pale mwili unapokuwa una nishati ya kutosha na hautaki kupoteza nishati ya ziada.

Nishati hii huhifadhiwa asilimia kubwa  katika mfumo wa glycogen mwilini mwako kwenye misuli, ini nk. Sasa inapotokea kiwango chako cha ulaji wa vyakula vya sukari ni kikubwa sana ndivyo kiwango kingi cha insulin kitatengenezwa na kumwagwa kwenye mzunguko wa damu kwenye kuhifadhi sukari ya ziada.

Kazi ya insulin sio kushusha sukari kama wengi tunavyofundishwa darasani! Kwa nini nasema hivi? Kazi ya insulin ni kuhifadhi nishati ya ziada kwa matumizi ya baadae na hivyo basi kupungua kwa sukari ni matokeo ya kazi ya insulin mwilini mwako.

Hebu soma na utafakari hapa

Umeingia katika chumba ambacho umekuta harufu mbaya sana ya deodorant spray au perfume. Punde tu utakapo ingia katika chumba hicho utasumbuka sana na harufu hio kwa muda mfupi na hatimaye unaizoea na kuona ni harufu ambayo haina madhara wala usumbufu kwako. Huu mfano utakusaidia kujua kwa nini tunasema insulin yako imeshindwa kufanya kazi na umepata kizuizi katika utendaji kazi wake.

Insulin kufeli kufanya kazi

Mwanzoni nimesema insulin hutolewa kwa kiwango kikubwa sana kulingana na kiwango cha sukari mwilini mwako. Kiwango hiki kingi cha insulin kwenye damu kwa muda mrefu inaweza kupelekea insulin kupoteza kazi yake kiuhalisia.

Na pia kitu kingine ambacho kinaweza kupelekea insulin kutofanya kazi ni vipokea insulin kutoitikia kwa sababu ya mafuta mabaya kuleta kizuizi katika vipokezi vya insulin. Vitendo vyote hivi viwili vinasababisha kiwango cha insulin kuwa juu wakati wote  na kama nilivyo eleza mwanzo kuwa kiwango cha insulin kinavyozidi kuwa kingi mwilini mwako kinashusha vichocheo vya Testosterone ambavyo ndio silaha yako mwanaume.

Sukari na wanga huongeza insulun

Hivyo basi ukiangalia katika maelezo haya utagundua kuwa ulaji wa vyakula na vinywaji vingi vya sukari vinasababisha kiwango cha insulin kuwa juu muda wote ambapo nacho kinapelekea vichocheo vya kiume kushuka na hatimaye unakumbwa na matatizo ya kukosa matamanio kwa jinsia tofauti, msongo wa mawazo, misuli kukosa nguvu muda wote umechoka, uzito kuongezeka kwa kasi sana na wengine hupelekea kumiliki vitambi.

Pia kiwango kingi cha insulin kwa muda mrefu kwenye damu kinaweza kupelekea kupata nywele usoni kwa wanawake, mwanaume kuishiwa vinyweleo sehemu kama kifuani, tumboni na maeneo mengine mengi.

3.Homoni ya Leptin

Hiki ni kichocheo cha pekee sana na huwa napenda sana kukizungumzia kwani kinaonesha jinsi gani binadamu alivyo umbwa kwa kutumia teknolojia ya uhandisi wa hali ya juu. Hiki ni kichecheo ambacho kinatengenezwa na seli zinazohifadhi mafuta ambazo zinapatikana kwa wingi kwenye misuli.

Kazi yake kubwa ni kupeleka ujumbe kwenye ubongo katika kuendesha hamu yako unapokuwa una chakula mbele yako. Na ubongo huitikia kwa kutoa taarifa ya kutosheka na chakula kwa kujihsi umeshiba na huwezi tena kuendelea na chakula.

Leptin na hamu ya kula

Sasa basi ulaji wa vyakula vingi bila mpango vyenye sukari nyingi unasababisha seli za kuhifadhi mafuta (fat cells) kutengeneza kwa wingi leptin ili kwenda kutimiza kazi yake. Kiwango cha insulin na leptin hupanda kwa pamoja kama mapacha vile. Hivyo hivyo kumbuka tafakari ile pale juu ya perfume.

Itafikia wakati kiwango kingi sana kinasababisha leptin kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi yake ya kukata hamu ya kula. Hivyo utakuwa una tatizo la kula mlo mkubwa bila kutosheka na ukitosheka muda si mrefu unahitaji tena kula. Hawa ndio watu wengi ni wahanga wa muda wote wanapenda kula vyakula vitamu vitamu tu, hamu haiishi (sugary addicted,sugar craving) .

Na wengi huishia kupata matitizo ya kiafya kama kuishiwa nguvu za kiume, uzito kupita kiasi, kitambi na kuishiwa nguvu kabisa ya misuli yote haya ni kwa sababu kiwango kingi cha leptin na insulin kinashusha vichocheo vyako vya testosterone.

4.Homoni ya Cortisol

Hiki ni kichocheo ambacho hutolewa na mwili pale unapokuwa katika hali yoyote ya mstuko ili kwenda kukabiliana na mshtuko huo.

Mfano labda mimi nilikuwa natembea njiani ghafla nikaona nyoka huyo mkubwa chatu. Mwili utastuka sana na kutoa vichecheo vinavyo enda kupambana na hio hali iliyoshtua mwili wako, mfano cortisol huenda kuongeza kiwango cha nishati ya mwili (glucose) kwenye damu na kuwa na nguvu ajabu ya kumkimbia adui yako aliyepo ,mbele yako.

Cortisol pia hutolewa hata kama mwili wako umekabiliwa na mstuko ndani kwa ndani. Mfano sukari mwilini imepungua mwili unatoa cortisol ambayo kazi yake kubwa ni kubadili ile nishati iliyokuwa imehifadhiwa katika mfumo wa glycogen kwenye misuli na ini kuwa sukari na hatimaye kuongeza sukari mwilini mwako.

Cortisol nyingi sana siyo salama

Sasa tafiti zinasema kwamba kiwango kingi cha cortisol kwenye damu kinachosababishwa na msongo, mstuko ndani ya miili yetu inayo endelea inasababisha Leptin kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi yake ipasavyo.

Na endapo leptin ikishindwa kufanya kazi yake ipasavyo utakuwa una tatizo la kula sana hasa vyakula na vinywaji  vya sukari bila hamu kukata na hatimaye kusababisha insulin kupanda juu na testosterone kushuka chini na hatimaye kuishiwa nguvu za kiume, matamanio kwa jinsia tofauti nk.

Hongera sana kwa kuendelea kusoma Makala hii, hapo juu nilitaka kukueleza tu nini kinatokea endapo unapatwa na upungufu wa nguvu za kiume kwani wengi mmekuwa mkinipigia simu kutaka kujua kwa nini nguvu za kiume sasa. Basi leo nazani umejifunza kitu, kama hujaungana nami katika ukurasa wangu facebook hebu bofya like maishadoctors uendelee kujifunza. Utafurahia makala zangu nyingi sana nzuri zimeandaliwa kwa ajili yako.

Basi napenda nikupe vitu vikuu 4 vinavyo angamiza watu kukosa nguvu za kiume hawa ndio maadui wako wakuu kuhusu tatizo lako hilo mpendwa, hebu endelea kusoma upate suluhisho lako,ufurahie ndoa yako,

Vitu 4 vinavyo angamiza nguvu zako za kiume na kukuacha mwenye msongo wa mawazo 

Najua utashangaa kuwa ni maadui ambao kila siku ni marafiki zako, na hujui kuwa wanaangamiza msingi wa ndoa yako. Ama inawezekana unajua lakini unayapuuzia haya tunayokufundisha kupitia elimu hii ya afya. Hivyo napenda kukuambia kuwa afya yako sio hazina ya milele linda sana afya kuliko vyovyote ulindavyo kwani ndio msingi wa furaha zote duniani.

1.Vinywaji vyenye sukari nyingi kama soda

Hivi ndio vimekuwa ni vinywaji vya kila siku hasa kwa wafanya kazi. Ndio maana wengi ndio wamekuwa wakisumbuka na matatizo haya ya kiafya kwani wanakula vyakula huwa napenda kuviita vya chapuchapu. Yani anataka soda ya kuvuta muda ili baadae akale.

Tayari nimeshaongelea jinsi gani sukari nyingi inashusha nguvu za kiume tena kwa kina zaidi. Wengine huuliza sasa Dr mimi siwezi kabisa kujizuia kunywa soda hata masaa tu, kwani kwenye friji zimejaa. Ni kweli huwezi kujizuia kwa sababu tayari umeshakuwa ni mlevi wa sukari (sugary addicted, sugary craving) .

Vyote hivi unaweza kujizuia kwa kukutana na mshauri wa afya lishe atakupa maelekezo mazuri namna gani unaweza kukata sugar craving kiurahisi kabisa. Kumbuka kiwango kimoja cha kichecheo kikivurugika vyote vinavurugika hivyo tunatakiwa kulinda sana kiwango cha insulin kuwa katika kiwango kizuri muda wote ili kufurahia ndoa zetu.

2.Kuepuka kabisa ulaji wa vyakula vya mafuta haya yale mazuri

Watu wengi sana huwa na fikra potofu kuwa chakula chochote cha mafuta ni kibaya, na hivyo hujizuia sana kula vyakula hivyo kwa kuogopa kunenepa. Napenda nikwambie kuwa hakuna adui mkubwa wa magonjwa yote kama SUKARI..

Vyakula vya sukari ndio chanzo cha magonjwa mengi ya tabia ambayo ni magonjwa sugu hapa duniani. Ndio chanzo cha uzito mkubwa kupita kiasi, kitambi, shinikizo la damu, kisukari, upungufu wa nguvu za kiume, uvimbe kwenye kizazi, mzunguko mbaya wa hedhi, ugumba,utasa nk.

Tafiti zinaonesha kuwa ulaji wa vyakula yenye mafuta kidogo sana inapelekea kupungua kwa vichocheo vya progesterone na kupelekea kupoteza nguvu za kiume na matamanio kwa jinsia tofauti. Pendelea kula vyakula vyenye mafuta mazuri kama nazi, karanga, ufuta, mayai na samaki.

3.Vyakula vyote vya kusindika viwandani

Napenda kusema kuwa ulaji wa vyakula hivi sio fahari kabisa, bali ni uzembe katika uandaaji chakula katika familia yako. Kuna usemi unasema kuwa, ukitaka uishi kwa bajeti kubwa katika familia yako, kula vyakula asili ambavyo babu zetu walikula enzi zile (EAT ORGANIC) Ndiomaana watu wengi hawapendi kula vyakula asili.

Wanatafuta vyakula vilivyo sindikwa kwani havina gharama kubwa. Unapokuwa upo jikoni unandaa chakula chako kwa familia yako, unatakiwa ujiulize kwa nini vyakula hivi vya kusindika vina bei rahisi kiasi  hiki?

Vyakula vya kusindikiza vinaharibu mazingira ya mwili

Ulaji wa vyakula hivi,siku zote huenda kuangamiza bakteria rafiki (Normal flora) pia wengi hupendelea kuita gut probiotics. Unapokuwa umewaangamiza hawa ndio chanzo cha magonjwa yote kwani katika makala zangu zilizopita nilieleza namna gani mfumo wa chakula unaweza kuwa chanzo cha afya bora yako, na chanzo cha magonjwa yote mwilini mwako.

Unakuwa ni mtu wakushambuliwa na maradhi nyemelezi yote na kudhoofisha ukuta wa mfumo wa chakula na hatimaye unaweza kuanza kupenyeza sumu (toxins), bakteria wabaya kama E. Coli. Vyakula ambavyo havijameng’enywa vizuri na protini zingine kama gluten ambazo ni hatari kwa afya yako.

Hivyo kama wewe umekuwa ukisumbuka na nguvu za kiume na umekuwa ni mlaji mzuri sana wa vyakula hivyo, hakikisha una viepuka. Kuwa mtu unayependa vyakula asili, vitarudisha uhalisia wa mfumo wako wako wa chakula kwa kuondoa tatizo la tumbo kujaa gesi na choo kuwa ngumu.

4.Sumu mbali mbali kutoka kwenye mazingira

Watu wengi sana wanapokuwa wanazungumzia tatizo la nguvu za kiume wanasahau kuhusisha mahusiano yaliyopo kati ya upungufu wa nguvu za kiume na mazingira yako. Najua kuwa tumekuwa tukijishughurisha na shughuli mbali mbali ambazo zinatufanya tugusane na sumu mbali mbali. Mfano madini ya mercury ambayo sasa yapo kila kona katika biashara zetu.

Madini ya lead haya ni madini mazito na hatari sana kwenye kudhoofisha utendaji kazi wa mwili wako, kukuletea msongo wa muda mefu na mengine mengi ambayo yanapelekea kupoteza nguvu za kiume. Kwa dunia ya sasa ya viwanda huwezi kuziepuka sumu kama hizi mwilini mwako, ni jukumu lako kuhakikisha unajijengea mazoea ya kuondoa sumu nzito hizi na mionzi mbali mbali katika mwili wako na hatimaye kuimarisha afya yako.

Najua umejifunza kwa nini sasa una upungufu wa nguvu za kiume au huna kabisa nguvu za kiume. Basi ningependa ijifunze jinsi gani unaweza kuhakikisha unaondokana na tatizo hili na ukafurahia ndoa yako na mahusiano yako kuanzia sasa, naomba basi nikuokoe katika tatizo hilo kwa kusoma njia tano za kurudisha nguvu za kiume.

Njia tano za kurudisha nguvu za kiume

Najua umekuwa ukisumbuka kila siku kufurahia ndoa yako, hadi imefikia hatua mbaya. Najua umekuwa mnyonge na mwoga wa kugundulika kwa mwenza wako kuwa unasumbuka na tatizo hilo. Umejaa woga, umegubikwa na msongo wa mawazo na umekuwa ukizunguka kila sehemu upate msaada na hatimaye umekuwa ukitoa pesa bila hata kurudisha furaha ya ndoa yako na nafsi yako!

Pole kwa changamoto lakini elimu ni bora kuliko yote yaliyokupata. Hebu soma hiki ambacho nimekuwa nikipewa asante kila siku na wagonjwa wangu wewe pia uwe miongoni mwao.

1.Epuka vinywaji vyote vyenye sukari nyingi,vya kusindika, vyenye vionjo vya sukari,rangi na ladha.

Katika afya yako kwani vyakula hivyo ni adui mkubwa sana wa afya yako hasa wakati unataka kurudisha nguvu za kiume. Kula vyakula asili, nafaka ambayo haijakobolewa,matunda kwa wingi ambayo hayasagwa yenye nyuzi nyuzi nyingi na pia juice ya matunda na mboga za majani. Utafurahia maisha ya kula vyakula asili na utafurahia ndoa yako. Anza kuanzia leo rafiki

Epuka pombe

Katika maisha yako yote kwani tafiti zinaonesha kwamba pombe inakupa hamu au shauku ya kufanya tendo la ndoa lakini inakunyima uwezo wa kufanya tendo la ndoa! Najua utashangaa lakini ndivyo ilivyo, kuna usemi wa kiingereza unasema,  “It provokes the desire, but it takes away the performance,”  Sio hayo tu pombe pia ni sumu, ni chanzo cha msongo wa mawazo  na kukupelekea kukosa kabisa hamu ya tendo la ndoa.

2.Fanya mazoezi ya kutosha.

Watu wengi wamelemewa na magonjwa kwa sababu tu mwili haupati damu ya kutosha kwenda sehemu mbali mbali kama vile ubongo, ini na figo. Viungo ambayo ndio sehemu zenye kuufanya mwili wako ufanye kazi katika uhalisia wake. Hivyo basi magonjwa mengi ya msunguko wa damu ni pamoja na nguvu za kiume kwani kama hufanyi mazoezi mwili wako unadhofika na kukosa uwezo wa kuhimili ndoa yako pia inapunguza nguvu za kiume.

Basi ningependa kusema kwa wale wazee siku hizi kuna vituo mbalimbali ambavyo vitakusaidia mwili wako kuwa imara na kurudisha uwezo wako katika tendo la ndoa kupitia mazoezi. Mazoezi huimarisha mwili wako na kuweka mbali mwili wako na maradhi mbalimbali yanayo sababishwa na uzembe.

3.Rudisha Virutubisho Vilivyopungua mwilini mwako

Hakikisha mwili wako unaupa madini ya msingi kama zinc, chuma, selenium, manganese na vitamin nyingi. Kwani madini haya ndiyo yanafanya mwili wako ufanye kazi katika kiwango stahiki kwani huwezesha viendesha shughuli za mwili yani enzymes kufanya kazi katika kiwango kizuri na kuimarisha mwili wako.

Unaweza kupata madini haya yote kutoka kwenye mboga za majani kama wewe ni mvivu basi unaweza kunywa juice inayotokana na mboga mboga kama kabeji,spinachi kale, nk. Kwa wale ambao ni kazi sana kuhimili zoezi hilo unaweza kujipatia kirutubisho hicho ofsini kwetu ambacho kina madini yote hayo.

4.Ondoa mafuta mabaya yanayopunguza mzunguko wa damu.

Unaweza kuondoa cholesterol mbaya mwilini mwako kwa kutumia mafuta ya omega 3 .Vyakula vyenye mafuta haya ni kama samaki, flaxseeds, na blackseeds. vyakula vyenye uwezo mkubwa wa kusafisha mafuta mabaya  mwilini mwako. Unaweza pia kufika ofsini kwetu kama utahitaji mafuta haya yaliyotengenezwa kitalamu utayapata na yatakusaidia.

5.Safisha Sumu mwilini kwa kutumia viondoa sumu.

Kuna sumu aina kuu tatu ambazo mimi huwa napenda kuziongelea siku zote na kushughurika nazo kwa wagonjwa wangu kama zifuatazo.

Sumu ambayo inatokana na mabaki ya hewa ya oksijeni yani free radicals ambayo ni moja wapo inaweza kuumiza seli za mwili wako na kusababisha seli zako kubadili mtazamo wa ukuaji na kuendelea kuzalishwa seli mbovu na hatimaye zinaweza kupelekea hata kupata kansa.

Sumu ambazo tunazipata kutoka katika mazingira yetu ya kazi kwa kukutana na metali nzito kama lead, na mercury ambazo ni kizuizi kikubwa sana katika utendaji wa mwili wako. Pia sumu inayotokana na mionzi mbalimbali inayotokana na kuchokozwa kwa miamba ya ardhi ( Earth’s crust)

Sumu inayotokana na vyakula tunavyokula ambavyo huenda na kuathiri mfumo wako wa chakula na hatimaye kuharibu ulizi wa mwili wako katika mfumo wa chakula. Afya yako huanzia katika mfumo wa chakula na magonjwa yote huanzia katika mfumo wa chakula. Unaweza kujaribu Detox package yetu ya siku 30.

GREEN HEALTH MALE SEX DRIVE PACKAGE

Green health male sex drive package

Tiba yetu ina combination ya dawa mbili za vig power na zinc tabltes zitakusaidia

  • Kuimarisha uwezo wa kufanya tendo la ndoa kwa kuchelewa mpaka dakika 20
  • Kuongeza uzalishaji wa mbegu(sperm count) na ubora wa mbegu(sperm quality)
  • Kuimarisha mzunguko wa damu kuelekea kweye uume na hivo kukufanya usichoke mapema unapofanya ngono
  • Inafaa kwa wanaume wote wanaowahi kufika kileleni, kukosa hamu ya tendo la ndoa na wanaoshindwa kuwapa mimba wanawake.

Gharama ya Tiba ni Tsh 150,000/= ambayo utaitumia kwa week 4 kudisha nguvu za kiume. Virutubisho na dawa zetu ni za asili zipo katika mfumo wa vidonge/capsules.

Najua umejifunza mengi sana kuhusu tatizo la nguvu za kiume, sasa napenda nihitimishe kwa kukuambia kuwa suluhisho la nguvu za kiume lipo kabisa ni kuhakikisha tu, unaliondoa tatizo hilo kwa kufuata elimu hii, na kama unaona elimu hii ni muhimu kwako basi unaweza pia kutupigia na kufika ofsini kwetu moja kwa moja kupata suluhisho la tatizo lako kwa Tsh laki 1 na 50 elfu tu..

Ushuhuda wa kupona changamoto ya nguvu za kiume

ushuhuda

Bilashaka nawewe unapenda kurejesha uwezo wa kufanya tendo kwa muda mrefu na uume kuwa imara sana kama huyu mtu. Usiache kututafuta ili urudishe tena heshima kwenye mahusiano yako

Ofisi zetu zipo Mwembechai Plaza, Magomeni Mwembechai,
Chati na Daktari kwa Whatsapp kupitia namba : 0678626254 kupata huduma , uwe mmoja wa mashuhuda wetu

Share and Enjoy !

Shares
Shares