Categories
Dondoo za afya

Kinachosababisha Meno kutoboka

mashimo kwenye meno

Tatizo la meno kutoboka au dental cavity kwa kitaalamu ni hali ya jino kuwa na shimo. Shimo kwenye jino huanza taratibu na huendelea kupanuka kama jino halitatibiwa mapema. Ni kutokana na kwamba kufanyika kwa shimo kwenye jino huwa haina maumivu kwenye kipindi cha awali inakuwa vigumu kujua kama tatizo lipo, ndio maana tunashauri kuonana na Daktari wa meno kila baada ya miezi mtatu akufanyie vipimo.
Pamoja na kwamba tayari umepata shimo kwenye jino na jino lako linaoza, fahamu kwamba kuna hatua unaweza kuchukua kuzuia hali hii isiendelee

Dalili za Meno Kutoboka

Dalili za meno kuwa na mashimo huwa inategemea na ukubwa wa tatizo la meno kuoza. dalili hizi ni kama

  • Meno kupata ganzi
  • Maumivu ya meno
  • Uwepo wa shimo kwenye jino
  • Utando mweusi kwenye meno

Nini Kinachangia Meno Kutoboka na Kuoza

Kutokana na maeleo ya Dr, Eddward Mellanby kuna vitu vinne vikuu ambavyo huchangia kwa meno kutoboka na kuoza

  1. Upungufu wa vitamini kwenye lishe (A, D, E na hasa vitamin D)
  2. Matumizi makubwa ya vyakula vyenye tindikali
  3. Upungufu wa madini kama (calcium, magnesium na phosphorus)
  4. Matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye sukari iliyosindkwa

Kila mtu na bakteria kwenye mdomo. Bakteria hawa hubadili mabaki ya vyakula mdomono kuwa tindikali. Na tindikali hii huanza kumomonyoa jino na kuruusu bakteria kushambuliza jino.Ndio maana tunashauri kusafisha meno kila baada ya kula au walau amara mbili kwa siku ili kuondoa mazingira ya bacteria wabaya kumea.

Makundi ya Watu waliopo kwenye Hatari zaidi ya Meno Kutoboka

  • Watu wenye matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye sukari na tindikali kwa wingi
  • Uchafu wa kinywa kama kutopiga brush vizuri
  • Watu wenye kukosa hamu ya kula na
  • Wagonjwa wa kiungulia ambapo asidi ya tumbo hurudi mpaka mdomoni.

Meno ambayo hutoboka zaidi ni yake ya mwisho yani magego. Meno haya yana uvungu na eneo pana kiasi kwamba linakamata kiurahisi mabaki ya vyakula.Meno haya ya magego hayasafishwi vizuri kutokana na ugumu wa kuyafikia ndio maaa yanakuwa kwenye hatari zaidi ya kuoza.

Hatua 4 za kufuata uzuia Meno kutoboka

Sasa na tuchambue zile sababu kuu nne ambazo zinachangia meno kutoboka na na hatua asili za kuchukua kulinda meno yako yasiendelee kuoza.

1.Epuka Sukari

Sukari ndio sababu namba 1 ya kutoboka kwa meno yako na pia ni chanzo cha magonjwa mengine mengi kama uzito mkubwa, kitambi, na kuvurugika kwa homoni.
Anza na kupambana na ulevi wa sukari, kwa kukaa mbali na vitu pmoja na soda na vyakula vya ngano. Tumia majani ya stevi kama kionjo cha kuongeza utamu kwenye kinywaji chako. Tumia pia asali mbichi kwa kiwango cha kati.

2.Tumia mazao ya maziwa na Vyakula vyenye virutubishi kwa wingi

Maziwa asili yana kiwango kikubwa cha vitamin na madini ambayo huimarisha afya ya meno. Ni muhimu kutumia maziwa asili walau mara mbili kwa week. Maziwa yana Calcium, Vitamin K2, Vitamin D3, magnesium na phosphorus. Mpangilio wa vyakula uwe kama huu

  • Vyakula vya wanyama kama supu ya mifupa, nyama na mayai
  • Mbogamboga kama spinach na mboga zenye kijani kilichokolea
  • Matunda kipande kimoja kila sikuVitamin D kutoka kwenye jua, nusu saa kila siku.
  • Vyakula vyenye mafuta mazuri kama mafuta ya nazi, nazi, parachichi, mafuta ya zeituni na samaki
  • Karanga, mbegu na maharage
  • Kutokula vyakula vilivyosindkwa, na fast food

3.Jaribu Coconut Oil Pulling

Njia hii iliyoanza kutumika kwa karne nyingi ili kusafisha kinywa na kuzuia meno kutoboka. Njia hii imekuwa ikitukuzwa sana katika uwezo wake wa kusafisha kinywa kwa kuweka mafuta mdomoni na kuyazungusha kisha kutema baada ya dakika 20.
Mafuta yana uwezo wa kuvuta na kunasa uchafu na vimelea wabaya waliopo mdomoni.
Soma vizuri hapa kuelewa kuhusu coconut oil pulling.

4. Punguza matumizi ya vyakula vinavyoongeza tindikali kama wanga uliokobolewa na kusafishwa, soda, juusi zilizosindikwa na pipi.

Maelezo ya mwisho

Matumizi ya mouth wash inaweza kuwa isiwe suluhisho la kudumu kwa kunuka mdomo au kuzuia meno yasioeze, mara nyingine mouthwash huongeza kunuka kwa mdomo, badala yake nashauri tumia njia asili na hakikisha unamwona daktari wa meno kila baada ya miezi mitatu.

Kuondoa maumivu ja jino lilotoboka tumia Peppermint

mint

Ni mafuta asili yaliyozalishwa nchini Pakistan. Yanasaidia kuondoa kabisa maumivu ya jino, na pia kuangamiza bakteria wabaya kwenye meno. Ni uhakika ukitumia tiba yetu hii ndani ya masaa mawili maumivu yanaisha na hayajirudii.

Gharama ni Tsh 25,000/= Tuandikie kwa whatsapp no 0678626254 kupata tiba hii

Bofya makala inayofuata: Kwanini unapata muwasho mkali mkunduni

Share and Enjoy !

Shares
Categories
Dondoo za afya

Kwanini Unanuka mdomo

Leo nataka kushea na wewe njia zangu rahisi jinsi gani uweze kutibu tatizo la kunuka mdomo, ikiwemo lishe na virutubisho vya kutumia katika program yako.

Kunuka mdomo ni hali ambayo kila mtu haipendi na moja ya matatizo ambayo watu huona aibu sana kuelezea. Lakini nataka nikwambie rafiki yangu unaesoma makala hii kwamba ukitaka kutibu tatizo la kunuka mdomo  inahitajika kufahamu chanzo cha tatizo hili.

Kikawaida kunuka mdomo kunasababishwa na kumea kwa bakteria wabaya kwenye mwili wako. Lkini kunuka mdomo ambako ni sugu na imekuwa ni hali ya muda mrefu husababishwa ukuaji kupita kiasi wa fangasi aina ya Candida kwenye mwili. Baadhi ya vyakula kama kitunguu saumu vinaweza kukupa ahueni ya muda mfupi . Nependa ufahamu kwamba kunuka mdomo si tu kwamba inaleta karaha bali pia ni kiashiria kwamba una tatizo kubwa la kiafya

Sababu Za Kunuka Mdomo

Karibu kila mmoja wetu hupata tatizo la kunuka mdomo katika muda fulani kwenye maisha yake. Wakati mwingine kisababisho kinaweza kuwa ni chakula ulichokula au aina ya bacteria wanaopatikana kwenye mdomo wako.

Harufu mabaya kwenye mdomo hutokea nyuma ya ulimi, kwenye koo na kwenye tonsils. Huku ndiko bacteria wabaya wanakozailiana na kutoa kemikali za Sulphur ambazo ndizo huleta harufu mbaya. Kwahiyo harufu mbaya mdomoni inaweza kusababishwa na ulaji wa vyakula vyenye Sulphur kwa wingi.

Ambapo kikawaida harufu hii huisha baada ya chakula kuchakatwa. Harufu mbaya mdomoni ya muda mrefu ni kiashiria cha uwepo wa tatizo la kiafya ambapo yaweza kuwa ni

  • Kutofanya usafi wa mdomo kwa makini
  • Lishe duni isiyo na virutubisho vya kutosha
  • Magonjwa ya fizi
  • Kuoza kwa meno na
  • Mataizo mengine ya kiafya kama kisukari au magonjwa ya ini

Ulaji wa vyakula hivi inaweza kuwa sababu ya kunuka mdomo kutokana na kwamba vizalisha kemikali nyingi ya Sulphur, vyakula hivi ni kama

  • Kitunguu maji na  kitunguu saumu: vyakula hivi huleta harufu kali zaidi hizo unatakiwa kuvitumia kwa tahadhari.
  • Vyakula vya sukari: sukari hupelekea kuoza kwa meno na kupelekea harufu mbaya mdomoni
  • Vinywaji vilivyosindikwa kama soda.

Hatua Tano za Kutibu tatizo la Harufu Mbaya Mdomoni

  1. Epuka kutumia vyakula vya sukari kwa wingi na nafaka kupita kiasi: hii ni ahtua ya kwanza katika kuelekea kuondoa harufu mbaya mdomoni, ambapo tunalenga katika kufata lishe ambayo ina kiwango kidogo cha sukari na nafaka. Vyakula hivi ni kama mikate, wali na bidhaa zingine za ngano. Hivo unapokula zaidi wanga fahamu kwamba unaenda kuvunjwa vunjwa na kubadilishwa kuwa katika mfumo wa sukari kitu ambacho ni mbolea kwa ukuaji wa fangasi na bacteria wabaya kwenye mwili wako
  2. Tumia vyakula vya mafuta zaidi(healthy fats) : badala ya kula wanga na sukari basi hakikisha unakula zaidi vyakula mafuta mazuri, mfano wa vyakula hivi ni kama parachichi, nazi, nyama , mayai na karanga. Mafuta ya nazi ya nazi yana lauric na Capric acid ambazo ni ni antibacterial yaani zinaua bacteria wabaya.kama una matatizo ini, mfuko wa bandama na figo.
  3. Tumia virutubisho zaidi. Unaweza kutembelea katika stoo yetu kwa kubonyeza hapa
  4. Tumia zaidi limau: limau na maji husaidia kwa kiasi kikubwa katika kuondoa harufu mbaya mdomoni. Unaweza kukata limau kisha ukanyonya maji yake, au ukaminya maji ya limau kwenye glass yenye maji kisha kunywa maji haya na yabaki mdomoni kwa muda wa dakika 10 kisha tema.

Kunywa maji ya kutosha: mdomo unapokuwa mkavu basi huongeza hatari ya kutoa harufu mbaya, kutokana na kwamba ukavu wa mdomo unapelekea kuzaliana kwa bacteria wabaya.

Coconut Oil Pulling

coconut oil pulling

Coconut oil pulling ni mja ya njia murua kabisa ya kusafisha bacteria wabaya mdomoni mwako na kukuacha na harufu nzuri ya kinywa sikuzote. ni njia salama na ya asili isiyohitaji matumizi ya kemikali mbaya wala dawa ambazo zina madhara makubwa.

Nimekuwa nikishauri mamia ya watu na wamefanikiwa kuondoa adha hii ya kunuka mdomo kupitia Coconut oili pulling, wewe pia unaweza kuwa mmoja wa mashuhuda wetu kama tu utazingatia kwa makini step za kufuata.

Uchafu na Vimelea Hutolewa Nje kupitia mafuta

Coconut oil pulling kama jina lake lilivyo ni kitendo cha kuvuta uchafu na bacteria ka vile sabauni inavyonyonya uchafu kwenye nguo wakati wa kufua nguo. Lakini kwenye upande wa kinywa unanyonya bacteria na uchafu kwenye meno kwa kutumia mafuta ya kupikia ya nazi.
Wenzetu wachina na nchi zingine kama India wamekuwa wakitumia njia hii tangu enzi za zamani katika kutibu matatizo kama

Kuoza kwa meno, kuondoa harufu mbaya kwenye kinywa, kuponya fizi zinazotoa damu, kuzuia magonjwa ya moyo, Kupunguza mcharuko mwilini (inflammation), Kusafisha meno kuwa meupe, Kuzuia magonjwa ya fizi, Kutibu lips kavu, Kuimarisha fizi na Kuondoa chunusi

Hatua 5 za Kufanya Coconut Oil Pulling

  1.  Hakikisha unafanya oil pulling asubuhi unapoamka kabla ya kula na kunywa kitu chochote
  2. Chukua kijiko kimoja au viwili vya mafuta ya kupikia ya nazi kisha weka mdomoni, anza kuzungusha ulimi na kuyasambaza mdomo wote taratibu kwa dakika 10 mpaka 20
  3. Baada ya muda huu tema uchafu wote bila kumeza hata kidogo kisha safisha mdomo na maji, unaweza kutumia maji yenye chumvi ili kuondoa mafuta yote. na hakikish usiteme kwenye sink tema nje ili kuzuia kuziba kwa mafuta kwenye sinki
  4. Brush meno yako kama kawaida
  5. Rudia kitendo hiki mara 3 mpaka 5 kwa week kupata matokeo mazuri zaidi.

Tiba Kupitia mafuta ya Peppermint

Mafuta ya mnanaa ama peppermint yanapatikana kupitia majani ya mmea wa mnanaa (Mentha piperita). Mmea huu hutumika hasa majumbani kama tiba asili ya matatizo ya tumbo.

Mafuta ya peppermint ni tiba asili na salama kwa changamoto ya kunuka mdomo na mezo kuoza. Huhitaji tena kuagiza nje ya nchi, tumekuletea mafuta salama yasiyochakachuliwa. Anza leo kutumia urudishe furaha yako.

Gharama ya Mafuta ya Peppermint ni Tsh 40,000/= Tuandikie kwa whatsapp no 0678626254

Share and Enjoy !

Shares
Shares