Categories
Dondoo za afya

Kujamba sana

Je ni salama Kujamba? au inategemea na Harufu?

kujamba sana

Wengi wetu lazima tumeshapitia hali ya kujamba sana kupita kiasi na kutukosesha raha. Japo kujamba ni kawaida na kila mtu anajamba kila siku, kuna watu wengine wanapata shida ya tumbo kujaa gesi na hivo kutoa gesi chafu mara kwa mara kuliko kawaida. Kitaalamu tatizo hili huitwa flatulence.

Ushuzi ni kitu gani

Ushuzi (fart) hutokana na gesi inayozalishwa tumboni kutokana na hewa tunayovuta na matokeo ya usagaji wa chakula tumboni. Kwahivo kutokea kwa ushuzi inaweza kutofautiana kwa kila mtu kutokana na mazingira na hali yake ya mwili.

Kama ambavyo umewahi kujishuhudia mwenyewe kuna wakati unajamba ushuzi wenye harufu mbaya. Wakati mwingine hakuna harufu, ama unaweza kujamba kwa sauti au pasiwe na sauti.

Mtu mzima mwenye afya anajamba mara 14 mpaka 18 kwa siku. Wakati mwingine anajamba hata bila kujijua kwasabau hakuna harufu au sauti.
Kwahivo unapotaka kuchambua hali ya afya yako ni muhimu zaidi kutazama harufu ya ushuzi na dalili zingine unazopata baada ya kujamba.

Je kuna jambo lolote la Kuhofia kuhusu Kujamba kwako?

Inaweza kuwa ndio au hapana,kwasababu wakati mwingine inategemea na aina ya chakula ulichokula. Mfano ukila vyakula vyenye kambakamba kwa wingi(high-fiber diet) na vyakula asili utapata ushuzi wa kawaida.

Lakini unapojamba kila mara kupita kiasi na ikiambatana na dalili zingine inaweza kuwa ni kiashiria kwamba kuna tatizo kwenye mfumo wako wa chakula. Tatizo hili laweza kuwa ni mabadiliko ya mazingira ya ndani ya tumbo (microbiome), kutokana na kukua kwa bakteria wabaya au fangasi.

Kilichopo kwenye Ushuzi

Fahamu kwamba ushuzi unatengenezwa kwa gesi, na gesi gesi kuu ni Nitrogen. Ambapo watafiti wanasema inachangia kwa asilimia 20 mpaka 90 ya gesi chafu inayotoka wakati umejamba.

Gesi zingine zinazounda ushuzi ni kama carbon dioxide ambayo huchangia asilimia 10 mpaka 30, oxygen ambayo huchangia aslimia 10, methane ambayo inachangia asilimia 10 na gesi ya hydrogen inachangia asilimia 10 mpaka 50.

Muunganiko wa gesi hizi ndio unaofanya harufu mbaya ya ushuzi kwasababu baadhi ya gesi zina kemikali ya sulphur ambayo ndio kiambata kinachotoa harufu. Sulphur hupatikana pia kwenye vyakula kama mayai na mboga kama kabeji.

Kwanini kuna utofauti wa asilimia za gesi zinazounda ushuzi na harufu?

Hii ni kwasababu hali ya ushuzi inatofautiana kwa mtu na mtu kutokana ni kiasi cha hewa aliyobugia, chakula alichokula na hali ya umeng’enyaji wa chakula tumboni.

Unaweza kushangaa ni kwanini unajamba lakini hakuna harufu mbaya inayotoka. Kiambata cha sulphur ndicho hufanya harufu kuwa mbaya zaidi ya kunuka. Asilimia moja tu ya sulphur inaweza kuleta harufu mbaya kwenye ushuzi. Kwahiyo kama aina ya chakula ulichokula kinategeneza sulphur kwa wingi basi ushuzi wako utakuwa unanuka.

Nini hasa kinasababisha Kujamba

Unaweza kuwa unajiuliza nini hasa hupelekea kujikusanya kwa gesi ambayo baadae unaitoa kwa njia ya kujamba. Japo visababishi vya ushuzi vinaweza kutofautiana kwa mtu na mtu lakini gesi inayotolewa ni ile ile haitofautiani.

Gesi iliyojikusanya tumboni hupita kwenye utumbo mdogo na baadae kutolewa nje kama unavyotoa haja kubwa. Wakati mwingine utoaji wa gesi hii unaweza kuambatana na maumivu hali inayoashiria pengine kuna chakula ulichokula kina tatizo. Au hakijachakatwa vizuri na hivo kuchacha.
Tatizo lingine kujaa gesi tumbo kikawaida huambatana na kujamba.

Baadhi ya sababu kwanini gesi inajikusanya tumboni mwako na kukupelekea kujamba ni pamoja na

  • Kumeza hewa (aerophagia): Hii inamaanisha kumeza hewa pasipo matarajio ambayo inajikusanya tumbo na kisha unaitoa kwa njia ya kujamba au kwikwi. Sababu mojawapo kwanini unabugia hewa tumboni ni kwasababu unakula chakula haraka au kutotafuna chakula vizuri kabla ya kukimeza. Kwahivo kama unaona wewe ni mtu wa kula haraka , jaribu kurekebisha tabia hii, tafuna taratibu ili usimeze hewa pamoja na chakula.
  • Kukusanyika kwa hewa chafu: Kujamba ushuzi unaonuka maranyingi hutokana na gesi inayozalishwa na bacteria waliopo kweye utumbo mpana baada ya uchafu ambayo haujafozwa kuchacha.
  • Mabadiliko ya mazingira ya ndani kwenye mfumo wa chakula (microflora): Fahamu kwamba katika mfumo wote wa chakula kuanzia mdomoni, kwenye koo, tumboni, mpaka kwenye utumbo kuna bacteria wazuri na wale wabaya. Bacteria wazuri wanasaidia katika uchaataji wa chakula na pia kama kinga dhidi ya athari za bacteria wabaya. sasa inapotokea bacteria wabaya wamakuwa wengi kuzidi wale wazuri ndipo utaanza kupata matatizo kama gesi tumboni na chakula kutosagwa.
  • Constipation(Kupata choo kigumu na kukosa choo kwa muda mrefu: Inaweza kusababisha mkusanyiko wa gesi chafu na kukupelekea kujamba sana kwasababu ukiwa na tatizo hili kasi ya mmen’genyo wa chakula inapungua.

Kwanini watu wengi wanajamba kwa sauti na wengine wanajamba polepole na harufu ni mbaya zaidi?

Hii yaweza kusababishwa na mpangilio wa misuli ya utumbo mpana na eneo la haja kubwa. Baadhi ya misuli inakusaidia kubana ushuzi na kuutoa taratibu pasipo sauti. Kama kila mara ukijamba sauti ni kubwa basi fahamu kwamba misuli ya eneo la haja kubwa(sphincter muscles) imelegea kiasi kiasi cha kuruhusu hewa kutoka bila ridhaa yako.

Je kujamba kuna Faida yoyote kwako? au kuna Madhara?

Kujamba ni kitu cha kawaida na moja ya njia ya mwili kutoa hewa chafu, kama vile tunavyopumua kutoa nje carbondioxide. Kwahivo kama unajamba usihisi kama ni jambo baya la kupambana nalo. Maana wakati mwingine kujamba kunaweza kuwa ni ulinzi na kwama tumbo lako linafanya kazi vizuri.

Vyakula vyenye kambakamba mfano matunda, mboga za majani, viazi, magimbi, uwele na ugali wa dona husababisha gesi kwenye mfumo wako. Lakini bado vyakula hivo vinatoa mbolea kwa bactetia wazuri kukua ambao watakukinga dhidi ya magonjwa kam saratani ya utumbo, kisukari, uzito mkubwa na kitambi na magonjwa ya moyo.

Kwa upande mwingine ni kwamba kama unajamba sana kupita kiasi, inaweza kuashiria kuna tatizo la tumbo matatizo haya ni kama

  • Mwili kukataa aina fulani ya chakula(Food intolerance)
  • Kutoboka kwa kuta za utumbo mwembamba(leay gut syndrome) na kusababisha sumu na vimelea kuingia kwenye mzunguko wa damu.
  • Kukua kwa vimelea kwenye utumbo/small intestinal bacteria overgrowth(SIBO).

Utajuaje kama kujamba kwako si kwa kawaida

Cheki kama kujamba kwako kunaambatana na dalili hizi ndipo uchukue hatua. Dalili hizi ni kama

  • Kukosa nguvu na uchovu
  • Ngozi kucharuka na kupata rashes au chunusi
  • Aleji mfano kutokwa machozi na koo kuwasha
  • Kuharisha na kukosa choo kwa muda mrefu au kupata choo kigumu
  • Kupata mkojo wenye damu au kinyesi chenye damu
  • Mumivu kwenye kwapa na katikati ya paja na viungo vya uzazi na
  • Mabadiliko ya joto la mwili, uzito, usingizi na mpangilio wa hedhi

Namna gani Upunguze Kujamba kupita kiasi

Haya ni matamanio ya kila mmoja wetu ili kupunguza aibu ya kujamba mara kwa mara pengine ukiwa na kundi la watu. Kitu cha kwanza kubadilisha ni lishe yako. Tumbo lako laweza kuwa linapata shida ya kuchakata aina flani ya vyakula au tumbo kuhifadhi zaidi sulphur, fangasi na bacteria.

Zoezi hili ni la kuajaribu maana watakiwa kufatilia ni aina gani ya chakula inakufanya kujamba sana, na siyo kila chakula kinaleta gesi kwa kila mtu. Baadhi ya vyakula vya kutizama zaidi ni kama

  • Maharage: Maharage ni chakula kikubwa ksababisha gesi kulio vingine. Ni kwasababu vimejaa aina ya wanga inayoitwa polysaccharides, ambayo inachacha kiurahisi inapoingia tumboni. Huhitaji kuacha kabisa kula maharage, ila fanya kuloweka kwenye maji usiku mmoja kabla ya kuyapika ili kupunza gesi inayozalishwa.
  • Maziwa na bidha za maziwa: kushindwa kumeng’enya maziwa (lactose intolerance) ni tatizo kubwa na linawapata watu wengi. Hii ni kwa bidhaa zote za maziwa. Bidhaa za maizwa zina aina ya sukari zinazouwa galactose na glucose amabazo ni ngumu kuchakatwa kiasi cha kupelekea gesi tumboni.
  • Mboga zenye sulphur: Mbona mboga zenye sulphur kwa wingi kama kundi la cruiferous, hapa kuna kabeji, broccoli na caulifolower huletekeza gesi kuliko mboga zozote zingine kwasabau zina kambakamba kwa wingi zaidi. Zinapopikwa gesi inapungua kiasi kuliko kuliwa mbichi.
  • Vyakula vilivyosindikwa ma kusafishwa(artificial, processed foods): Baadhi ya vyakula vya viwandani vyenye mafuta mabaya vinaweza kuwa vigumu kuchakatwa na hivo kupelekea gesi tumboni. Lenga kula vyakula asili na kutumia mafuta mazuri kama ya nazi na oilve kama kiungo cha kupikia. Kadiri unavokula vyakula asili nivyo unarahisishia kazi tumbo kusaga chakula vizuri.

Badili Mtindo wa Maisha ili Kupunguza Tatizo la Kujamba kwa

  • Kufuta kwenye lishe yako vyakula ambavyo siyo rafiki.
  • Tumia virutubishi (probiotics) ambavyo vitasaidia kurudia bacteria wazuri tumboni. Vyakula hivi ni kama maziwa asili ya mtindi na sprulina.
  • Weka vionjo kwenye lishe yako: Vionjo hivi husaidia kuimarisha usagaji wa chakula na kuua vimelea wabaya tumboni. Vionjo hivi ni kama manjano(tumeric), tangawizi, mdalasini na pilipili.
  • Fanya mazoezi na kunywa maji ya kutosha: Vyote hivi kwa pamoja vitakusaidia kutoa uchafu nje ya mwili na kusafirisha virutubishi ndani ya mwili. Mazoezi ya squats ni muhimu zaidi.

Kama una tatizo la kujamba sana. Muhimu tukupatie Chai tiba ya intestine Cleansing. Itakusaidia kusafisha tumbo na kurekebisha mazingira ya mfumo wa chakula.

intestine cleansing tea

Chai tiba hii ni Tsh 50,000/= tu. Tuandikie kwa whatsapp no 0678626254 kuanza tiba.

Bofya kusoma: Chanzo cha kubanwa pumzi na kifua

Share and Enjoy !

Shares
Categories
Dondoo za afya

Kutokwa Jasho Jingi lenye Harufu

kutokwa jasho jingi

Maelezo ya utangulizi

Ni kawaida kila mtu anatokwa na jasho kweye mwili. Kutokwa jasho ni hali ya mwili kujipooza na kuzuia kupanda kwa joto la mwili kupita kiasi. Kwahivo mwili unapopambana kubalansi joto lako la mwili ndipo hapo utaanza kutokwa na majasho. Inapotokea unapata jasho jingi na linatoka pasipo joto la ndani ya mwili kuongezeka hapo ndipo tunasema una tatizo, ambalo kitaalamu linaitwa hyperrhidrosis.

Watu wenye tatizo hili hutokwa na jasho jingi kipindi ambacho mwili hauhitaji kupoozwa.
Tatizo hupunguza sana hali ya mtu kujithamini kwasababu linakera na kusumbua. Dalili za jasho jingi zinatofautiana kwa watu na ni tatizo
la kurithiwa kwa vinasaba kutoka kizazi kimoja hata kingine. Tatizo hili tunaweza kuligawanya katika makundi mawili

Primary Hyperhidrosis

Aina hii ya kutokwa jasho jingi huanzia utotoni au kipindi cha balehe na hutokea kwenye maeneo kadhaa ya mwili hasa kwenye miguu, paji la uso na kwenye kwapa. Mara nyingi kwa kesi hii mtu huaanza kutokwa jasho jingi baada tu ya kuamka kitandani.

Secondary Hyperhidrosis

Aina hii ni pale mtu anapotokwa na jasho jingi mwili mzima na unaweza kupata dalili hizi hata kama umelala. Chanzo chake yaweza kuwa tatizo flani la kiafya linalokusumbua au matumizi ya dawa.
Hali ya jasho jingi inakera na yaweza kukukwamisha kufanya shughuli zako za msingi mfano kufungua kurasa za kitambu, kufungua mlango au kushukilia kitu.

Sababu na vihatarishi vinavyopelekea mtu kutokwa jasho jingi ni pamoja na

  • Kuugua kisukari
  • Kukoma hedhi
  • Maambukizi
  • Msongo wa mawazo
  • Ugojwa wa gauti
  • Tezi ya pituitari kufanya kazi zaidi (hyperpituitarism)
  • Ujauzito
  • Athari ya sumu kama metali nzito mfano mercury
  • Uzito mkubwa na kitambi
  • Uvimbe
  • Kushuka kwa kiwango cha sukari kuliko kawaida kwenye damu (hypoglycemia)
  • Matumizi vyakula na vinywaji vyenye caffeine kama kahawa
  • Matumizi ya aina fulani za vidonge
  • Kuzaliwa kwenye familia yenye historia ya kuugua tatizo hili na
  • Pombe

Hatua 3 za Kutibu na Kupunguza kutokwa jasho jingi.

  1. Weka mwili katika hali ya usafi muda wote
    Hakikisha unaosha vizuri na kukausha miguu inayonuka,kwapa zenye jasho na maeneo mengine ya mwili zenye athari. Ili kuzia maambukizi kwenye ngozi yenye unyevunyevu hakikisha unatumia sabuni zilizotengenezwa kwa siki au vinegar ya apple au mafuta ya tea tree, na witch hazel, yatasaidia kuzuia maambukizi ya fangasi na bacteria kwenye ngozi.
  2. Vidonge vya Soy power na Zinc kwa wanawake
    Kama chanzo cha tatizo lako ni kukoma hedhi, basi hakikisha unatumia vidonge vya Soy power na zinc viakusaidia kupunguza dalili za kukoma hedhi kama kutokwa ana jasho usiku na mwili kuchoka sana unaweza kuagiza hapa.
  3. Jaribu njia mbalimbali za kupunguza msongo wa mwanzo, kwa kufanya mazoezi kama yoga, tahajudi (meditiation)

ANGALIZO

Kutokwa jasho jingi yaweza kuwa siyo tatizo kubwa lakini linaweza kuathiri uwezo wako wa kufanya shughuli za kimaisha.Kwa nyongeza kama tulivoona pale awali kupata jasho jingi inaweza kusababishwa na tatizo kubwa la kiafya ambalo unatakiwa kushughulika nalo, kama kisukari, uvimbe na athari ya sumu kama metali nzito.
Unapotumia njia kama marashi, au pafyumu ili kupunguza harufu na wingi wa jasho basi hakikisha unasoma kwanza kuhusu athari zake.a

Share and Enjoy !

Shares
Categories
Dondoo za afya

Kwanini Kisimi kinawasha na Kuvimba?

Utangulizi kuhusu Kisimi

Kisimi au kinembe ni kiungo kinachoonekana mwanzoni mwa uke kwa juu, kazi ya kiungo hiki ni kuchochea hisia na kumfanywa mwanamke kufikia kilele katika tendo la ndoa. Kisimi kinaweza kuonekana kidogo kwa juu lakini napenda ufahamu kwamba kisimi kimejichimbia zaidi kueekea ndani kama mzizi na ni kiungo kikubwa.

Kwenye makala hii, tutazungumzia changamoto kadhaa wanazopata wanawake kama kisimi kuvimba, kupanuka, na kuwasha. Endelea kusoma kufahamu zaidi.

Je kuna Size Sahihi ya Kisimi?

Japo hakuna kiwango cha kawaida cha kisimi, lakini najua wafahamu kiwango au size ya kila siku ya kisimi chako. Mara kadhaa kuna baadhi ya hali au shughuli huweza kusababisha kuvimba kwa kisimi kwa muda flani mfano kuongezeka kwa hisia za mapenzi, na kuna sababu zinazoweza kupelekea kuvimba kwa kisimi kwa muda mrefu.

Kuvimba kisimi kwa siku chache

Kuvimba kisimi kwa mda mfupi ni kawaida kama mwanamke ameamshwa kihisia. Hisia za kimapenzi zinapokuwa juu,mzunguko wa damu huongezeka kuelekea kwenye via vya uzazi. Kisimi pamoja na mashavu ya uke huongezeka ukubwa katika hichi kipindi, na kupungua ukishafika kileleni.
Kama mwili wako unasisimuliwa mara kwa mara kimapenzi, na usifike kileleni, basi kisimi kinaweza kuendelea kuwa kimetutumka kwa mda mrefu zaidi.
Vitu vimngine ikiwemo maambukizi vinaweza kuwa chanzo cha kuvimba kwa kisimi pamoja na mashavu ya uke. Mashavu ya uke yanaweza kuvimba kutokana na
Aleji na vifaa au kemikali, nguo, cream au manukato
Maambukizi ya fangasi na bacteria
Kupiga punyeto na kuingiliwa na kitu kwa muda mrefu kwenye uke.

Kuvimba kisimi kwa Zaidi ya wiki

Kama tatizo linafikia wiki moja na zaidi linaweza kuwa limesababishwa na

Matatizo ya homoni

Kuwa na homoni nyingi za kiume (androgens) kama testosterone huweza kupelekea kisimi kuongezeka ukubwa.

  • Wanawake wenye polycystic ovarian syndrome (PCOS) na matatizo mengine ya homoni wanapata changamoto hii ya kukua kwa kisimi.
  • Vimbe kwenye Mayai (Ovarian Tumors)
  • Uvimbe kwenye mifuko ya mayai huanza kuzalisha homoni za kiume kwa wingi na hivo kuepelekea kuongezeka kwa ukubwa wa kisimi.

Lini unatakiwa Kumwona Daktari

kama kisimi au kinembe chako hakirudi katika hali ya kawaida ndani ya siku mja basi unatakiwa kumwona daktari. Unatakiwa pia kumwona daktari kama unapata dalili zingimne kama maumivu na kutokwa na majimaji aidha damu au uchafu. Ni kwa sababu dalili hizi zinaweza kuashiria maambukizi kwenye uke.Hakikisha unamwona daktari unapoona tu dalili zisizo za kawaida. Usisubiri mpaka tatizo liwe kubwa.

Tuandikie kwa whatsapp no 0678626254 kuchati na daktari

Bofya makala inayofuata: Kwanini unalia baada ya tendo la ndoa

Share and Enjoy !

Shares
Categories
Dondoo za afya

Kinachosababisha Meno kutoboka

mashimo kwenye meno

Tatizo la meno kutoboka au dental cavity kwa kitaalamu ni hali ya jino kuwa na shimo. Shimo kwenye jino huanza taratibu na huendelea kupanuka kama jino halitatibiwa mapema. Ni kutokana na kwamba kufanyika kwa shimo kwenye jino huwa haina maumivu kwenye kipindi cha awali inakuwa vigumu kujua kama tatizo lipo, ndio maana tunashauri kuonana na Daktari wa meno kila baada ya miezi mtatu akufanyie vipimo.
Pamoja na kwamba tayari umepata shimo kwenye jino na jino lako linaoza, fahamu kwamba kuna hatua unaweza kuchukua kuzuia hali hii isiendelee

Dalili za Meno Kutoboka

Dalili za meno kuwa na mashimo huwa inategemea na ukubwa wa tatizo la meno kuoza. dalili hizi ni kama

  • Meno kupata ganzi
  • Maumivu ya meno
  • Uwepo wa shimo kwenye jino
  • Utando mweusi kwenye meno

Nini Kinachangia Meno Kutoboka na Kuoza

Kutokana na maeleo ya Dr, Eddward Mellanby kuna vitu vinne vikuu ambavyo huchangia kwa meno kutoboka na kuoza

  1. Upungufu wa vitamini kwenye lishe (A, D, E na hasa vitamin D)
  2. Matumizi makubwa ya vyakula vyenye tindikali
  3. Upungufu wa madini kama (calcium, magnesium na phosphorus)
  4. Matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye sukari iliyosindkwa

Kila mtu na bakteria kwenye mdomo. Bakteria hawa hubadili mabaki ya vyakula mdomono kuwa tindikali. Na tindikali hii huanza kumomonyoa jino na kuruusu bakteria kushambuliza jino.Ndio maana tunashauri kusafisha meno kila baada ya kula au walau amara mbili kwa siku ili kuondoa mazingira ya bacteria wabaya kumea.

Makundi ya Watu waliopo kwenye Hatari zaidi ya Meno Kutoboka

  • Watu wenye matumizi ya vyakula na vinywaji vyenye sukari na tindikali kwa wingi
  • Uchafu wa kinywa kama kutopiga brush vizuri
  • Watu wenye kukosa hamu ya kula na
  • Wagonjwa wa kiungulia ambapo asidi ya tumbo hurudi mpaka mdomoni.

Meno ambayo hutoboka zaidi ni yake ya mwisho yani magego. Meno haya yana uvungu na eneo pana kiasi kwamba linakamata kiurahisi mabaki ya vyakula.Meno haya ya magego hayasafishwi vizuri kutokana na ugumu wa kuyafikia ndio maaa yanakuwa kwenye hatari zaidi ya kuoza.

Hatua 4 za kufuata uzuia Meno kutoboka

Sasa na tuchambue zile sababu kuu nne ambazo zinachangia meno kutoboka na na hatua asili za kuchukua kulinda meno yako yasiendelee kuoza.

1.Epuka Sukari

Sukari ndio sababu namba 1 ya kutoboka kwa meno yako na pia ni chanzo cha magonjwa mengine mengi kama uzito mkubwa, kitambi, na kuvurugika kwa homoni.
Anza na kupambana na ulevi wa sukari, kwa kukaa mbali na vitu pmoja na soda na vyakula vya ngano. Tumia majani ya stevi kama kionjo cha kuongeza utamu kwenye kinywaji chako. Tumia pia asali mbichi kwa kiwango cha kati.

2.Tumia mazao ya maziwa na Vyakula vyenye virutubishi kwa wingi

Maziwa asili yana kiwango kikubwa cha vitamin na madini ambayo huimarisha afya ya meno. Ni muhimu kutumia maziwa asili walau mara mbili kwa week. Maziwa yana Calcium, Vitamin K2, Vitamin D3, magnesium na phosphorus. Mpangilio wa vyakula uwe kama huu

  • Vyakula vya wanyama kama supu ya mifupa, nyama na mayai
  • Mbogamboga kama spinach na mboga zenye kijani kilichokolea
  • Matunda kipande kimoja kila sikuVitamin D kutoka kwenye jua, nusu saa kila siku.
  • Vyakula vyenye mafuta mazuri kama mafuta ya nazi, nazi, parachichi, mafuta ya zeituni na samaki
  • Karanga, mbegu na maharage
  • Kutokula vyakula vilivyosindkwa, na fast food

3.Jaribu Coconut Oil Pulling

Njia hii iliyoanza kutumika kwa karne nyingi ili kusafisha kinywa na kuzuia meno kutoboka. Njia hii imekuwa ikitukuzwa sana katika uwezo wake wa kusafisha kinywa kwa kuweka mafuta mdomoni na kuyazungusha kisha kutema baada ya dakika 20.
Mafuta yana uwezo wa kuvuta na kunasa uchafu na vimelea wabaya waliopo mdomoni.
Soma vizuri hapa kuelewa kuhusu coconut oil pulling.

4. Punguza matumizi ya vyakula vinavyoongeza tindikali kama wanga uliokobolewa na kusafishwa, soda, juusi zilizosindikwa na pipi.

Maelezo ya mwisho

Matumizi ya mouth wash inaweza kuwa isiwe suluhisho la kudumu kwa kunuka mdomo au kuzuia meno yasioeze, mara nyingine mouthwash huongeza kunuka kwa mdomo, badala yake nashauri tumia njia asili na hakikisha unamwona daktari wa meno kila baada ya miezi mitatu.

Kuondoa maumivu ja jino lilotoboka tumia Peppermint

mint

Ni mafuta asili yaliyozalishwa nchini Pakistan. Yanasaidia kuondoa kabisa maumivu ya jino, na pia kuangamiza bakteria wabaya kwenye meno. Ni uhakika ukitumia tiba yetu hii ndani ya masaa mawili maumivu yanaisha na hayajirudii.

Gharama ni Tsh 25,000/= Tuandikie kwa whatsapp no 0678626254 kupata tiba hii

Bofya makala inayofuata: Kwanini unapata muwasho mkali mkunduni

Share and Enjoy !

Shares
Shares